TAIZÉ

Kuimba kwa tafakari

 

Kuimaba ni kitu cha muhimu sana katika kumtolea Mungu sifa. Kuimba nyimbo fupi, kwa kurudia rudia, huzifanya za tafakari. Kwa kutumia maneno machache nyimbo hizi huonyesha msingi wa kweli wa imani, ambao haraka haraka huingia na kukaa akilini. Jinsi ambavyo maneno yanaimbwa kwa mara nyingi, ukweli huu hupenya taratibu ndani ya ubinadamu wetu mzima. Kwa hiyo kuimba kwa kutafakari kunakuwa njia yetu ya kumsikiliza Mungu. Kunamruhusu kila mmoja wetu kushiriki kwa pamoja wakati wa sala na kubaki pamoja katika utulivu tukimsubiri Mungu, bila kuhitaji kujiwekea muda maalumu kwa uhakika sana.

Kufungua njia za kumuamini Mungu, hakuna kinachoweza kukaa badala ya sauti nzuri za binadamu zilizounganishwa pamoja katika nyimbo. Uzuri huu unaweza kutuonjesha chembe za “furaha za mbinguni tukiwa duniani”, kama Wakristu wa Mashariki wanavyoiweka. Na maisha ya ndani yanaanza kuchanua na kung’ara ndani yetu.

Pia nyimbo hizi husaidia muendelezo wa sala za binafsi. Kwa kupitia nyimbo hizi, kidogokidogo, ubinadabu wetu hupata umoja nadani yetu na Mungu. Zinaweza kuendelea katika ukimya wa mioyo yetu wakati tukiwa kazini, tunapoongea na wengine, au tukiwa tumepumzika. Kwa namna hii sala na maisha ya kila siku ni kitu kimoja. Zinatuwezesha kuendelea kusali katika ukimya wa mioyo yetu, hata tukiwa hatutambui.

“Nyimbo za Taizé” zinachapishwa katika lugha tofauti tofauti na rahisi, hata hivyo maandalizi yanahitajika ili kuzitumia wakati wa sala. Maandalizi haya ni vizuri yakifanyika kabla ya sala yenyewe, ili sala yenyewe ikianza hali ibaki kuwa tulivu na ya kuruhusu tafakari.

Wakati wa sala ni vizuri kama kunakuwa hakuna mtu anayeongoza nyimbo, kwa namna hii kila mtu anaweza kutazama msalaba, alama za picha au altare. (hata hivyo, kwenye mkusanyiko mkubwa sana, inaweza kulazimu mtu mmoja kuongoza, Pia, kwa umakini mkubwa sana, kikundi kidogo cha vifaa vya muziki au waimbaji wanao saidia kutia nguvu wengine, wanaweza kuimba, isipokua daima wakumbuke kuwa hawafanyi maonyesho kwa wengine). Mtu anaye anzisha nyimbo kwa ujumla anakuwa mbele sehemu ya juu, pamoja na wale watakaosoma zaburi, masomo na maombi/sala za waumini (the intercessions), siyo wakiwaangalia wengine bali wakiangalia upande uleule kuelekea altare au alama ya picha. Kwani nyimbo zikianzishwa tu hivihivi, sauti itakua ya chini sana. ‘A turning fork or pitch pipe’ vinaweza kusaidia, au vyombo vya muziki kutoa nota ya kwanza au kusindikiza sauti. Na kuhakikisha kasi ya wimbo haiwi ndogo sana, kama inavyotokea wimbo ukiimbwa kwa muda mrefu. Kadiri idadi ya washiriki wa sala inavyoongezeka, kunakua na umuhimu wa kutumia kipaza sauti, na ingefaa zaidi kilongalonga cha kushika kwa mkono, kwa ajili ya kuanzishia na kumalizia wimbo (Wimbo unaweza kumalizwa kwa kuimba “amina” katika nota ya mwisho). Mtu anaye anzisha wimbo anaweza kuwasaidia wengine kwa kuimba kwenye kipaza sauti, lakini kwa uangalifu ili asimeze sauti za wengine. Mfumo mzuri wa sauti ni muhimu kama mkusanyiko ni mkubwa; kama ni muhimu kuukagua, ukaguliwe kabla ya sala na fanya majaribio na wale watakao tumia.

Nyimbo zilizoko katika lugha mbalimbali ni mwafaka kwa mkusanyiko unaohusisha mataifa mbalimbali toka dunia nzima. Kwa sala zinazo husisha watu wa rika zote kutoka maeneo ya jirani, ni vizuri nyimbo nyingi ziwe katika lugha inayoeleweka na baadhi ya washiriki, au kwa kilatini. Kama inawezekana kila mtu apewe karatasi au kitabu cha nyimbo. Inawezekana pia kuweka nyimbo moja au mbili zinazojulikana vizuri kwa eneo hilo.

Vyombo vya muziki: Gita au kinanda chaweza kusaidia mpangilio mzuri wa nyimbo. Ni vya msaada mkubwa sana katika kuhakikisha sauti si ya juu/chini sana na kasi ya wimbo ni ya kawaida. Gita lipigwe katika mtindo wa ‘classical’ na siyo katika mtindo wa ‘folk style’. Kipaza sauti kinaweza kuwa cha muhimu ili vyombo visikike. Kama nyongeza ya hivi ambayo ni vya msingi, kuna vifaa vingine vya kusaidia katika vyombo vya muziki.

Ilirekebishwa mara ya mwisho: 14 August 2007

“Jambo la kustaajibisha sana hapa Taizé ni kwamba utaratibu huu wa viitikio vya utulivu umechukuliwa katika liturjia, na ya kwamba, hautumiki tu katika sala za binafsi bali hata katika sala za jumuiya. Baadhi ya vijana ambao pengine hawafahamu kabisa kuhusu fumbo hili huanza kujifunza kusali”.

Olivier Clément