TAIZÉ

Vijana na sala Taizé

 
Mmoja wa mabruda anaangalia ni namna gani vijana wanajihusisha na sala; anatazama sala katika mapana yake ndani ya Taizé, na kwake yeye anaiona kama kitu kinachowakumbusha vijana mara kwa mara kutafuta ukweli juu ya kitu fulani.

Mara tatu kila siku, kila kitu husimamishwa kwenye kilima cha Taizé: kazi, masomo ya biblia, majadiliano katika vikundi vidogo vidogo. Kengele zinaita kila mmoja kwenda kanisani kwa ajili ya sala.Mamia, na wakati mwingine maelfu ya vijana kutoka nchi nyingi ulimwenguni wanasali na kuimba pamoja na mabruda wa jumuiya. Nyimbo fupi huimbwa kwa kurudiwarudiwa, na kwa maneno machache, msingi halisi huoneshwa ambao huingia akilini kirahisi. Baada ya hapo biblia inasomwa katika lugha mbalimbali. Katikati ya sala, kipindi cha ukimya hutawala kwa muda, ambacho hutoa fursa ya pekee kabisa na ya aina yake ya kuonana na Mungu.

Sisi mabruda mara kwa mara tunafarijika sana, tunavyoona kuwa kumbe vijana wengi wanaweza kubaki kanisani kwetu wakiomba, wakati mwingine masaa kadhaa, kukiwa kimya au wakati mwingine kukiwa na sauti ndogo ya nyimbo zinazo saidia tafakari. Wakati mwingine wao wenyewe wanashangaa kugundua ni kwa kiasi gani wamesali wakiwa Taizé. Tunapouliza vikundi ambavyo viko katika siku za mwisho kukaa Taizé, ni kitu gani kimewagusa kuliko vyote, jibu la haraka haraka linalokuja bila kufikiri wala kusitasita: “sala”! Na zaidi ya hapo ni wangapi kati ya wale wanaokuja na kutueleza kwa uchangamfu mkubwa kuwa kwa mara ya kwanza wameweza kusali kama watu “wazoefu wa sala”! hicho ndicho kinachotugusa zaidi.

Sisi wenyewe, tunazidi kushangazwa na hili, Ni kitu gani kinachowawezesha vijana kuwa wazi katika majadiliano ya ndani kabisa kwenye sala? Ni kwa namna gani tunaweza kuwafanya wagundue hayo, hata bila kujua namna ya kusali, hata bila kujua ni kipi cha kuomba au kipi cha kutarajia, Mungu alisha tuwekea shauku ya ushirika?

Hata bila kuweza kujibu maswali haya, naweza kutaja kuwa sala za Taizé ambazo kwangu mimi zinaonekana kama kitu kinachowakumbusha vijana kutafuta ukweli juu ya kitu fulani: Sala rahisi kwa mtu yeyote, sala ya tafakari, sala ya moyoni.

Sala rahisi kwa mtu yeyote

Sala ya jumuiya imebadilika kidogo sana kwa muda wa miaka mingi sasa; imeendelea kuwa rahisi. Bruda Roger mara zote alitaka kusiwe na kitu chochote kwenye sala ambacho si kirahisi. Kwake yeye kusoma kifungu ambacho ni kirefu sana au kigumu kingewafanya watu kushindwa kuhisi ule upendo wa roho mtakatifu ndani ya sala.

Kule kutaka undani wa sala kugusa idadi kubwa ya watu, ndiko kulikofanya jumuiya iandae utaratibu wa kusali kwa kuimba nyimbo rahisi za tafakari. Siyo kuwa kila kitu kiliandaliwa kwa ajili ya kuwazoesha vijana. Kwa namna moja au nyingine, mapambio ya Taizé yenyewe siyo nyimbo zilizo andikwa katika mtindo wa muziki wa vijana. Naamini kabisa kuwa nyimbo zetu zimetengenezwa kwa mtindo wa aina yake. Kwa misamiati yake, ambayo ni ile ya zaburi, desturi ya muda mrefu ya uimbaji wa sala ulioanza mwanzoni mwa mikutano ya Israeli. Kwa sifa zake za kutafakarika na kujirudia rudia. Kimsingi, jumuiya ilianza kwa kuimba zaburi na hata sasa hufanya hivyo. Isipokuwa badala ya kuimba zaburi yote, tunakazia kifungu fulani, tukikitafakari kwa pamoja, tukikifanya kitukumbushe na kutupatia uzoefu ambao utatuleta katika mwanga.

Kinachowagusa vijana hapa Taizé labda ni kule kujitahidi kwetu kufanya muonekano wa imani kuwa katika hali ya urahisi kadiri inavyowezekana, na wakati huohuo bila kupoteza msingi wake. Vijana Wanajisikia (wenyewe bila kufundishwa) kuwa sala zilizopendekezwa kwa ajili yao, zaidi sio kuwa zimetafthiriwa katika lugha zao wenyewe, kwamba ni za kigeni, badala yake mwaliko wa kutafuta kweli ambao huwafanya kusema maneno kwa vinywa vyao zaidi ya uwezo wao, ambayo taratibu huwalazimisha kujiachia na kujiweka katika hali nzuri na tayari kwa ajili ya Mungu. Vijana ni wazuri sana katika kugundua hili, wanaweza kutofautisha kati ya mawazo waliyojijazia wenyewe na mambo ya kweli na kuaminika. Labda wanagundua kwamba kuweka sala zetu kulingana nao, tunataka kama jumuiya, kupanua njia zetu kwa wote kwa ajili ya ukaribu tunaotaka kuishi na Mungu. Kwa maana hiyo basi, ni muhimu sana kuwa uimbaji dama hufanywa na wote na siyo kumwachia kiongozi au waimbaji wachache na kuacha kiitikio pekee kiimbwe na mkusanyiko wote.

Sala ya tafakari

Sala na nyimbo za Taizé pia ni tafakari za biblia. Huwa nashangazwa sana wakati wa siku zote za watakatifu, wakati ambao kanisa letu linakuwa limejazwa na wanafunzi wa sekondari za ufaransa kugundua ni kwa vipi bila kufundishwa vijana 2,500 wanaimba maneno kama “Naomba nishangilie na kufurahia upendo wako!” kutoka katika nyimbo zilizoandikwa hivi karibuni kwa lugha ya kifaransa. Nina hisia kuwa, kwa kurudia rudia kifungu kimoja au viwili, wimbo huwafungulia moja kwa moja kwenye Neno la Mungu na kuwawezesha kuingiwa na kuuweka ndani yao uzuri na “ukali” wa maneno ya biblia. Na hivyo, wakati sasa neno liko moyoni na kugunduliwa tena kwa kusoma, baadhi ya vifungu humulikwa kwa mwanga usiotarajiwa.

Wakati mwingine nashangaa kama uimbaji wetu siyo namna ya kuingiza ‘lectio divina’, ile namna ya kusoma Neno kwa usikivu mkubwa ambao hutoa nafasi ya kufanya kifungu kieleweke kwa mapana yake na kumuingia mtu na kumkaa kwa muda mrefu. Wayahudi huzungumzia “kuchambua” sheria. Mmoja wa walimu wa sheria wa kiyahudi alinukuliwa katika mkusanyiko wa vitabu vya kiyahudi toka baada ya karne ya kwanza ya kristu akisema, “geuza msahafu huku na huku, kwani kila kitu kimeandikwa humo; wenyewe utakupa ufahamu/ujuzi wa kweli. Jiimarishe katika somo hilo na kamwe usiliache; hamna kizuri uwezacho kukifanya”(Mishna Aboth 5,26). Hapa Taizé, kurudiwarudiwa kwa nyimbo kunatukumbusha uchambuzi huu, pumzi hii ya Neno.

Sala ya moyoni

Upande mwingine ambao hunigusa mara kwa mara ninapowasikiliza vijana wakizungumzia sala hapa Taizé ni ule uwezo ambao huupata wakati wa kipindi cha ukimya katikati ya ibada ambao huwapatia nafasi ya kujichunguza ndani mwao. Wanajua kuelezea ni vipi ukimya unawawezesha: “kuchunguza/kufanya hesabu ya mambo yote yaliyopita”, “kusikiliza moyo wako”, “kufikiria juu ya matatizo yako”, “kuondoa mawozo”, “kujipumzisha”, “kufanya utafiti juu ya nafsi yako”, “kuchukua nafasi ya kuwa wewe kama wewe/kuvaa utu wako”,... Wakiwa pamoja, hawaogopeshwi na ukimya. Kinyume na hayo, wengi wanasema mwanzoni dakika kumi zilionekana kama muda mrefu sana, lakini baadaye, walijikuta kuona kama kitu cha kawaida.

Nashangaa kama kile wanachojaribu kukiweta katika maneno hakishabihiani na kile wakristu wa mashariki wanachokiita “sala ya moyoni” na pia “kukesha kwa ajili ya kujiweka tayari”, “linda moyo wako kwa uangalifu wote”, kitabu cha methali chasema, “maana humu hutoka chemichemi ya uzima.” (Methali 4:23).

Katika biblia moyo ni kitu cha katikati kwa binadamu, muhimili ambao nguvu zote hutegemea/hukusanywa. Kwa mabruda wenye utamaduni wa mashariki, kusali kwa kurudia rudia vifungu vya maneno vilivyoambatanishwa na mpangilio maalumu wa vipindi vya kupumzika, ndicho kitu cha kwanza na kikubwa kwenye sala ya moyoni, kwa maneno mengine, jitihada za kuweka nguvu katika umoja na kuziwezesha kupita katika moto mkali moyoni na katika chungu cha upendo. Kwa kufanya hisia, na nguvu zetu kuwa kitu kimoja, moyo ni sehemu ambayo, nia zuri zaweza kutokea kama yalivyo maji masafi. Sala kama kitu kinachoweza kutufanya waangalifu, kuwa macho na kusikiliza, hutuwezesha kufikiri kwa undani, kupangillia tena mahitaji yetu na kuyaambatanisha na upendo. Sala ni yale maandalizi ya moyo kuwa tayari kupokea tahadhari ambayo upendo huhitaji katika namna mbalimabali.

Kupitia kuimba na ukimya, vijana wanagundua kwamba wanaweza kuwa na mioyo mipya, moyo usio na matata, katika uhalisia wa neno, moyo mkunjufu. Wakristu wa mwazo walizungumzia sala kama njia ya kuyeyusha “mafuta ya kiroho” ambayo huelemea fikira zetu na mahitaji yetu. Taswira za watu unaoshirikiana nao katika mambo ya Mungu, nazo huelezea kitu hicho hicho: Moyo mkunjufu ni moyo ambao huangalia mambo ya msingi, moyo ambao daima uko karibu na matakwa yake, na kwa namna hii hugundua waziwazi ni namna gani Mungu anataka moyo huo uwe. “kila hitaji ndani yetu ambalo linaelekezwa kwa Mungu tayari ni sala. Kile unachotamani kuwa nacho tayari ni sala yako. Kuna sala ya ndani ambayo kamwe haikomi.”(Mtakatifu Augustino anajadili juu ya zaburi 37.)

Pia kwa kuwa wazi na bila kuzuiliwa, moyo hujifunza kukomaza maamuzi na uwezo wetu wa kung’amua, njia ya namna ya kuishi. Vivyo hivyo kufahamu mambo ambayo ni tata na ambayo fikira zetu zilifikia mwisho. Kwa namna hii naamini kuwa vijana wanaweza kuelewa kuwa “sala haitufanyi kuwa duni katika dunia. Kinyume chake, hakuna jukumu kubwa kuliko kusali. Kwa namna ambavyo tunajifanyia wenyewe sala rahisi na ya upole, ndivyo tunavyoelekezwa katika upendo na kuuonyesha katika maisha yetu. Bruda Roger, “Barua 2005, nyakati za amani zijazo”.

Kwa mapana haya ya sala tunayo jaribu kushiriki na vijana: “kutoa nafasi ndani ya moyo” wa mtu, “kuchambua” kifungu cha maandiko na kusikiliza moyo “kwa makini/tahadhari”, hitaji letu la ndani kabisa ni kuwafanya wawe na ufahamu juu ya imani kubwa aliyotuachia Bruda Roger katika barua yake ya mwisho ya “barua ambayo haijamalizika” unfinished letter:

“Mungu anabaki kuwa upande wetu hata katika ukiwa wetu usioelezeka. Mungu husema kwa kila mtu, ‘umzuri na unafaa sana mbele ya macho yangu, nakuthamini sana na ninakupenda’. Kweli, katika yote Mungu anayoweza kufanya ni kutoa upendo wake; Hii inahitimisha injili katika ujumla wake.”

Ilirekebishwa mara ya mwisho: 14 August 2007

Sala na Nyimbo

Kuelewa sala za Taizé, sikiliza nyimbo, soma muziki na jikuze katika ukimya.